Alipitia mengi yanayohitajika ili kuwa mchanaji hasa. Alipata msaada kutoka kwa wasanii wakongwe wa hip hop ya Tanzania kama akina Lindu Lindulu, Zavara Mponjika, Saigon na wengine wengi tu. Kwenye mwaka wa 2009 alifanya mahojiano ya nguvu na Saigon wakati huo mtangazaji katika kipindi cha "HIP-HOP Base" cha EATV. Mahojiano haya Nash aliongea mengi ya msingi kuhusu uwanja wa hip-hop na alivyorudi katika kuchana alikuwa tofauti na zamani kabisa. Baadaye akaja kutoa "Nani Mkali Kwenye Game" chini ya mtayarishaji Kita ndani Ramo Records huko Magomeni, Dar es Salaam. Hiyo ilikuwa mwaka 2010. Mwaka 2011 anatoa kandamseto ya kwanza "Hazina Sura ya Kwanza" halafu akaendelea kutoa albamu kila mwaka uliofuata hadi 2014. Mwaka wa 2012 "Mzimu wa Shaaban Robert", mwaka wa 2013 "Chizi", mwaka wa 2014 Mchochezi. Albamu zote zimetazamia maisha halisi ya raia wa Tanzania na Afrika kwa ujumla jinsi wanavyopitia magumu yao ya kila siku.[1]